Bab Kubwa

Katika pitia pitia yangu kwenye tovuti nilikutana na e mail huria ya walimu kupigwa viboko. waungwana hebu someni halaf kama una muda changieni. What does this mean to us. What do you think about these things happening katika nchi yetu . " Siasa ya Uhuru na Umoja" karne ya 21. I am lost.


Ama kweli usipoona ya Musa utaona ya Farao.
Hivi kweli bado watanzania tuna pioneer kuwapa watumishi wa serikali
adhabu ya viboko kwa kutowajibika ipasavyo?
Mbona mimi naona watumishi wa serikali na mashirika ya umma kama
asilimia 95 mnastahili kupata viboko kila siku?
Tena tunaanzia watumishi wa ikulu na kisha tunashuka kuja chini. Tena
hawa wakuu wa wilaya hao ndio usiseme maana hata Prime Minister
aliyepita alishawambia kukitokea njaa watawajibishwa na sasa njaa ipo
kila sehemu wala sioni lolote. Sijui tungeanzia kwao?
By the way hawa wakuu wa wilaya kazi zao ni zipi hasa? ni viranja? mi
nadhani hata bila hawa kama watu wana nidhamu ya kazi kazi zitakwenda.
Hawana kazi hawa mbali na kuwa tax users tu. Lakini nimefuatilia
nyendo za watanzania woooote including walio katika ajira za serikali
na wanaojiajiri kwa kweli watu hawafanyi kazi ipasavyo.
Watanzania wengi upenda anasa sana kuliko kazi. Nashangaa utaona saa
4asubuhi baa zimejaa watu wanakunywa pombe. Na hapo hujaenda baa za
pombe zinaitwa za kienyeji. Huko wamejaa puuuuuuu.
Sasa tuanzie kuchapa nani? Ukienda Polisi utachapa wote kuanzia IGP.
Maana kama sivyo angeshamchapa na kumfukuza kazi Abdalah Msika.
Ukienda jeshini uko ndiko usiseme ufisadi wa pesa za umma kibao. Nenda
benki kuu ambako wezi hawakuchapwa viboko. Nenda hospitalini, huko
ndiko usiseme watu wengi wanakufa kwa ujinga wetu tu. Sasa nani
atapona fimbo hizi.?
Kwa nini watu wamepoint waalimu peke yao? system nzima ya serikali iko
hoi. Hakuna malengo ya kazi. Watu hawajitumi.
Nilikuwa siku za karibuni nikiuguza ndugu yangu katika hospitali ya
mkoa fulani hapa Tanzania. Kila mahali pachafu. Ward aliyolazwa
haikuwahi kufagiliwa siku zote 14 alizokuwapo huyo mgonjwa wangu kiasi
kwamba wagonjwa wenye nafuu na wasaidizi wao walifanya zamu kupiga
deki sakafu na kusafisha choo.
Shuka hazikuwa zikibadiliswa wala kufuliwa na bado wagonjwa
hawakuruhusiwa kuweka shuka zao binafsi eti si sheria. Vyandarua
vilikuwa vimejaa matobo.
Dawa hazikuwapo hadi ukanunue na adha nyingi nyingi tu je hawa nao
wapate viboko?
Mbona walimu wanaonewa kila kitu??????
Mi napendekeza wote waliopelekwa mahakamani kwa ufisadi nao wachapwe
kwanza ndio wapelekwe mahakamani.
Huu mtindo wa kishenzi ulioanzishwa na hawa wapiga soga wa kitanzania
toka SISI M. mnawaita ma DC wa kupiga watu si wa kiungwana. Huyu
Yamungu anamkejeli Rais wake wazi wazi na baadhi hapa tunaona anafanya
sawa. Mimi sijui kiongozi wake huyo analionaje. Lakini hizi hukumu
tunazozitoa nje ya sheria ni ushenzi sawa na jinsi tunavyoua albino au
wezi mitaani hata kama tunaona hii ndio sawa. Hakuna tena sheria kila
mtu anafanya analoona.
Tukomeshe hivi vitendo vya kijinga na tufuate sheria.
Mtumishi wa umma akikosea zipo sheria za ajira anazotakiwa kukabiliana
nazo sawa na Mr mheshimiwa sana Mnali alivyokutana nazo. Au na yeye
alitakiwa apate kiboko? Mambo ya kuchapana fimbo ni ya kijinga maana
hata walimu sasa hawatumii fimbo kama adhabu kwa wanafunzi wao. Iweje
wao wapate adhabu hii? Mnali na Yamungu wote si waungwana ila natumia
neno moja tu kama sifa yao. Ni washenzi. Mark you hili si tusi ila ni
sifa yao. Maana washenzi ni watu wasiokuwa na ustaarabu.

Share

Reply to This

Replies to This Discussion

safari bongo ni ndefu dada yangu , lakini naamini pamoja tutaweza ipo siku , lakini Nashukuru Mungu kuwa watu tunafunguka macho kama hivi umeeka mjadala huu kwenye mtandao nasi twapata kuona mtazamo wa wengi

Kazi nzuri !!!

Reply to This

Hapo umenena "Mpendwa.
Kwakweli Taifa letu kwa wakati huu linakabiliwa na changamoto kubwa sana.

1) Tishio la kukatika kwa umeme kwa kipindi kirefu
11) Ufisadi katika kila nyanja za Serikali
111) Mauaji ya Albino

Na yote hayo yanasababishwa na kuwepo kwa viongozi wengi wasio na utashi Nchini kwetu.

Reply to This

hureeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee,
Big up sana sister kwa mdahalo wako mtamu mbaya. Me naona ile adhabu waliopewa walimu ingerudi kwa
mkuu wa wilaya mwenyewe coz aliwadhalilisha sana.
Kama kuna waajiriwa wanaonyanyaswa kwa kila idara bac cwengine bali ni matcha coz wenyewe ndiyo wanawandaa mawaziri, marais pia wakuu wa wilaya but wanapewa mshahara mdogo na FIMBO juu, huu c udhalilishaji kabisa jamaniiiiiiiiiii?

Reply to This

Big up sana sister kwa mdahalo. Alichokifanya DC kwa kuwachapa Matcha viboko ni udhalilishaji na sipendi litokee au kurudiwa na angesitahiri DC apewe adhabu kali kuwa Fundisho kwa waliobaki, Unamwadhibu Ticha mbele ya madenti anatarajia kesho yake ticha angemfundisha huyo Denti aelewe.

Tchao,
Chax.

Reply to This

kweli mimi nimekukubali sana tu dada yaani sasa hivi taifa letu limekwesha

Reply to This

KUWACHAPA WALIMU VIBOKO NI NOMA KWELI

AU INAWEZEKANA HUYO JAMAA ALIKUWA ANALIPIZA KISASI KAMA YEYE ALIVYOCHAPWA AKIWA MDOGO

Reply to This

KAKANANII said:
KUWACHAPA WALIMU VIBOKO NI NOMA KWELI

AU INAWEZEKANA HUYO JAMAA ALIKUWA ANALIPIZA KISASI KAMA YEYE ALIVYOCHAPWA AKIWA MDOGO

Reply to This

sema, sema, sema, bring it!!!!!!!!!!!!!!

Macho said:
Hapo umenena "Mpendwa.
Kwakweli Taifa letu kwa wakati huu linakabiliwa na changamoto kubwa sana.

1) Tishio la kukatika kwa umeme kwa kipindi kirefu
11) Ufisadi katika kila nyanja za Serikali
111) Mauaji ya Albino

Na yote hayo yanasababishwa na kuwepo kwa viongozi wengi wasio na utashi Nchini kwetu.

Reply to This

uongozi wa kweli na muelekeo wa nchi yetu ulizikwa pamoja na Mwalimu Nyerere( kiongozi wa ukweli), na kamanda wake Kwawawa-offcourse! habari kama hizi zina umiza moyo sana hasa kwa sisi ambao hatupo nyumbani, hao waliochapa walimu dada naomba unisendie mimi niwachape wao!! tu-endelee ku-expose hawa mapimbi!! nchi yetu deserves BETTER!!!!!

Pa1

Reply to This

yaani dada umewaza jambo la maaana sana kwani kufanya hivyo ni ukosefu wa elimu,fikira,na fadhila pia kwani hebu tukae na kufikiri kwamakini sana bila ya elimu kutakuwa na serikali bora.
hebu na hao viongozi nao wafikiri bila ya walimu wangeupata uongozi silazima akusomeshe mwalimu fulani hapana bwana mwalimu ni mwalimu tu wote thaini yao ni sawa.
kwakweli hapo serekali imechemsha sana kuwashusha thamani walimu.
yaani thamani ya mwalimu nitofauti na yamtu yoyote yule hebu aulizwe huyo alotoa adhabu hiyo yeye kafundishwa na nani adi akawa na kauli ya kusema walimu wachapwe viboko. lazima atanza na kuseme mwalimu fulani sio fulani kamwe.

dada umejadili jambo lenye mana sanaaaaaaaaaaa
nakupongeza sana kwa utafiti wako.

Reply to This

Hongera sana sister kwa kutoa mjadala huu
kweli tabia ya kuchukua sheria mkononi siyo fair
kwani ingelikuwa hivyo tunge malizana na TZ asi
ngelibaki mtu.
Nashauri sheria iwe inatumika na sio ubabe.

Reply to This

Kwanza napenda kukupongeza kwa your article, maana huo ujumbe me nauita article, coz kila kitu ukisemacho hapo juu dada yangu i`ts so true.. nasikitika sana kuona nchi yenye mali nyingi za kujivunia but bado tuko nyuma sana kwa kimaendeleo, na ninashangaa sana kuona vitu kama mbuga za wanyama, zinamilikiwa na wazungu, why tunawaachia watu hao wamiliki mali zetu, kwanini serekali isimiliki vitu kama hivyo coz vinatuiingizia hela nchini, watu wanapokuja utalii. na huu ni mfano mdogo sana, kuna vitu vingi sn ambavyo ni utajiri wa nchi yetu lakini wazungu wanamiliki, na bado tunajiita eti tuko huru, wakoloni bado wako, na wanazidi kuongezeka..wa tanzania fungueni macho...mi niko nchi za nnje, navitu ninavyoona huku, ningependa kuona vitu kama hivi tz..watanzania tumeendekeza raha na sinaa, haswa kazini, na ndomana tuko nyuma kimaendeleo. mtu unaenda bar kunywa huku uko kazini, hio kweli inaendana? unaendesha umelewa? kweli hio unaweza kuita responsibility? na kuwapiga walimu fimbo, nivitu vyakipuuzi, waanze kujipiga wenyewe..

Reply to This

Reply to This

RSS

About

Bab Kubwa Media Bab Kubwa Media created this social network on Ning.

Tovuti bora. Sikiliza mziki wa Bongo popote Ulipo. Pata ladha ya Bongo. Chat, Photos, Videos & The latest and greatest Bongo Flava. Enjoy!



Forum

Ummussalaam

Who Cheats More? Men or Women 8 Replies

Started by Ummussalaam in General. Last reply by PinkCoffee 18 hours ago.

KAKANANII

ETI JAMANI KWANINI BONGO HAIENDELEI 11 Replies

Started by KAKANANII in General. Last reply by Arnold K. T. K. 1 day ago.

Zulekha

Walimu kuchapwa viboko 12 Replies

Started by Zulekha in General. Last reply by jojo Nov 19.

Said de Markson

UNDUGU MUHIMU

Started by Said de Markson in General Nov 6.

john bart

what a man got to do now:? 5 Replies

Started by john bart in General. Last reply by sarah ibrahim Oct 29.

mathias makunguru

ngono ya jinsia moja siyo.

Started by mathias makunguru in General Oct 13.

Ellinaza A.Killonzo

BBA REVOLUTION

Started by Ellinaza A.Killonzo in General Oct 10.

raul

mama wa kambo 2

Started by raul in General Sep 30.

mick john

KUFULIA C ISHU

Started by mick john in General Sep 25.

Boscow M. Maiso

Tanzanians Life 1 Reply

Started by Boscow M. Maiso in General. Last reply by Bab Kubwa Media Sep 12.

samson justo

nothing than lov

Started by samson justo in Lonely Hearts! Sep 11.

john bart

we can do it

Started by john bart in General Aug 31.

Hussein

wuold like to get to know u 4 Replies

Started by Hussein in Lonely Hearts!. Last reply by Hussein Aug 14.

yusuf mohammed khiranga lumumba

Hapo Cha Cha!!!!!!!!!!!!!

Started by yusuf mohammed khiranga lumumba in General Aug 13.

Robert frank mawalla

Hi.

Started by Robert frank mawalla in General Aug 9.

jmo

jmo

Started by jmo in General Aug 1.

raul

kitendawili mapenzi

Started by raul in General Jul 17.

Hardson Sanga

SECEND CHANCE 1 Reply

Started by Hardson Sanga in General. Last reply by Hardson Sanga Jul 14.

© 2009   Created by Bab Kubwa Media on Ning.   Create Your Own Social Network

Badges  |  Report an Issue  |  Privacy  |  Terms of Service

Sign in to chat!